Tuesday, November 12, 2013

Jumanne Weds Dyness....@ Mwenge Social Hall

Katika kanisa la RC, Tabata la Mt Anwarite, waili hawa wakala kiapo cha maisha. Wakiwa na tabasamu zao za asili, Mtanashati Jumanne na kipenzi chake wa siku nyingi na rafiki yake wa ukweli,Dyness, Wakasindikizwa na ndugu na marafiki zao hapo na kwa furaha isiyopomika, wawili hao wakaacha baba na mama zao na kuambatana pamoujar.
 
Uhondo ukanoga hapo na kama vile haukutosha, mambo ikahamia kwa ukumbi maarufu hapo Mwenge Dar es Salaam, waitwa Mwenge Social Hall-Kumbi Pacha na Mwik Social Hall wa pale Sinza. Hapo mambo yakawa baam baaam!!
 
Mtaalam wa fani, Dj Ndende akatulia hapo na chatter yake ya Respect DJs. Akawapagawisha na wakapagawaaaaa. Katikati, bila ajizi, sauti ya ukweli ikarinima ikiwakaribisha na kuwatabasamisha maharusi na wageni wengine hapo ndani, mwaanzo mpaka mwisho....heheiyaaa; mwendo mdundo...Tupooogo, bado tupooogo...tunachopata chocho mi na yeye tuuu, kiwe kidooogo, kikubwa ni majaliwa......" zikashuka za kikurya, za ijita, gospoooz...ikaja baak to baak...kitu ya I have been thinking about you...tukasogea mpaka DRC na kujiachia na mzee Koffi Antonio Olomide...tukaenda hadi Nigeria na kukutana na zileeeee za Personally!!! oh oh...tukavinjari mitaaya pwani ya mashariki ya Africa na kujiachia n taarabu na miduara...wataka nini tena!!
 
songa nasi hapa kwa picha
 
Rangi: Silver na Peach



 
 

Tuesday, November 5, 2013

Pius Ntiga weds Neema @ Landmark Hotels...

Ilikua ni furaha sana kwa maharusi wale, Pius Ntiga na rafiki yake Bi Neema, mtoto wa kichagga. Shamrashamra zilianzia kuleee nyumbani kwa kaka yake na Bw Harusi, ambaye pia amekua ni mlezi wake tangu Enzi za sekondari Dr na Mrs Peter Mgosha. Baadaye wasukuma wale wakahaia katika kanisa la RC pale Msimbazi Centre. Hapo Mtanashati Pius akasahau mambo yake kutoka kule Uhuru FM na kumuhakikishia Neema wake kuwa wataishi milele mpaka kifo kitakapowatenganisha.
 
Utamu haukuishia hapo, uhondo halisi zikahamia paleeee Landmark Hotels chini ya Combination ya hatari ya McNdimbo na Dj Ndende kutoka Respect Djs (shereheyetu.blogspot.com). Hapo haikua kazi ngumu kuweka vichwa zaidi ya mia tatu katika usalama wa burudani kutoka mwanzo hadi mwisho.
 
Huku akiwapo Paschal Mwaja na kuongoza waleee watanashati kutoka The 15 Family, marafiki na majirani wa ukweli wa Dr & Mrs Peter Mgosha, Mlezi wa Bwana Harusi; Machilika, Simba, Nyambere, Karokola, Deo, Hamidu, Saburi, Tamara, Pendo, Faith, Mama Kamila na wengineo....na huku yupo Mamaaa Angel na Crew nzima ya Uhuru FM...moto uliwaka pale. Full maburudaaani ng'wanawane...zikaanza ndombolo ya solo, sebene, gospoooz, kwaito na taarab za ukweli...wataka nini tena banaaaaah
 
Songa nasi kwa picha hapa:

Picture na Video by LaserLooks Production (0763835478)
 
Rangi: Maroon na Gold