Thursday, January 23, 2014

EDA ASIMWE 2014 SPECIAL!! @ DUNKEEN HOUSE...

Akiwa na tabasamu la asili na kile mumewe mtarajiwa alichokiita "She looks Mmmmmmwaaaah", Bi Eda Asimwe, huku akisindikizwa na rafikiye mkyuut Irene, alijongea taratiiib ndani ya Ukumbi wa Dunkeen House, Mikocheni nakupokelewa kwa hamasa na nduguze wale kutoka Karagwena wengine wa nchi jirani.
Vijana wa HB Entertainmwnt wakatia chachandu katika chuzi la shughuli na kukoleza habari za kutoka Karagwe na kuweka uhalisia wa asili yake Bi Eda.
Bila ajizi wala shubiri, Mtanashati DJ Ndende, akawa nyuma ya mashine na kutoa budani isochosha kutoka Respect Djs (www.shereheyetu.blogspot.com) na kuwasha moto wa uhakika; kuanzia na kwaito, sebene, gospooz na mibongo ya fuleva ya kumwaga...achilia mbali zileeee za asili. Haposauti ilotulia ya mdau wenu ikiweka sawia utaratibu mzima wa shughuli ilopendeza haswaaa.
songa nasi kwa picha hapa
Colors: Pink na Silver

Saturday, January 4, 2014

Nkunzi 2014 Special At Kiramuu Hall

Nderemo na vifijo vilisikika kwa haja pale ndani ya ukumbi wa ukweli: KIRAMUU Hall, Mbezi Beach Dar es Salaam, pale ambapo mtoto wa kiha, binti wa zamani wa PCM pale Kilakala, Eng. Nkunzi James Nyabakari alipokua akiingia kwa tabasamu la haja!! Huku akisindikizwa na rafiki yake kipenzi, Lyidya kwa pembeni, Engineer Nkunzi wa Tanrod akatembea kwa maringo na urefu wake mithili ya twiga, akanyanyua mkono juu kwa madaha na kuwasalimia ndugu, jamaa na marafiki waliojazana kushuhudia kuagwa kwake. Raaaaha Mustarehe.

Ngugu zaqke, waha wale wakapagawishwa na uhondo wa nyimbo za kwao "...indegeee inooobhobhaaa...." na vionjo vya Upendo Nkone katika lugha yake ya asili. Dj Ndende kutoka Respect Djs, akawapoteza na wakapotea kabisaa.
Kampani yake ya PCM-Kilakala; Neema Kisha, Reme, Hekima, Irene Lucian, Dorothy, Ney Opiyo, Rita, Rose na Rachel wakawa nae kwa karibu wakimshangilia Engineer mwenzao huyo.
Mabest wengine, Watanashati wa Mujiiiini, wakiongozwa na Madam Chairperson; Leyla Bhanji na Admini Adel(McDouble A) ambaye alikua pia mshenga, Lizzy, Joanita, Jamila kutoka Kilombero na Mdau McNdimbo...wakalifanya tabasamu la Nkunzi lisikauke kabisaa mpaka usiku mkubwa shughuli ilipogota kwa ukingo. Ilikua ni shidaaaaah!!

Songa nasi kwa picha
Colors: Aqua Green, hot pink na Silver