Tuesday, August 27, 2013

What a Wedding! Davis Nyanda weds Martha Kisandu

Furaha na nderemo za kutosha kutoka kwa wasukuma wa pande mbili; The Nyandas na The Kisandus zilisikika kila pembe kufuatia kijana mtanashati, mpole na mwenye uzelendo wa kisukuma hasaaa, Davis Nyanda alipofunga pingu za maisha na kipenzi chake, Bi Martha Kisandu pale kanisa la RC na baadae pale Maua Social Hall, Ubungo External.

Mwalimu huyo, mtaalamu wa lugha kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam, alisindikizwa na wana Idara wenzake wa Idara ya Fasihi; Bw Emmanuel Lema na Bi Elizabeth Kweka na wengine kutoka Idara ya Lugha Za Kigeni na Isimu hapo UDSM.

Huku ukumbi ukiwa umependeza kweeli kweli na kukiwa na kiyoyozi cha haja hapo, wageni waalikwa walihakikishiwa burudani na wabobevu katika fani; McNdimbo Crew wakiwa na Kwayu Music Classic ikiongozwa na DJ Baby...ilikua ni noumar!!!

Wasukuma wakapata yao, wakristo wakapata yao, wazee wa zamani wakapoozwa na yao, vijana na enzi zao wakapata yao na hata vijana wa dot com wakarushwa ile mbayaaa. Watake nini tena. Kikwetukwetu, burudani ndio jadi yetu sieee; YOUR SATISFACTION IS OUR PASSION.

Songa nasi kimatukio kwa picha

Colours: Green na Orange



Friday, August 2, 2013

Julianus to Esther! Utawapenda!!!!

Ooooooh oooooooh My God is gooood oooh!! Eeeeeeeeh.....eeehh eeeeehhh, my God is goood oooh!! Everything is double double!!! Shuka chini....chini tenaaaa....one two threee!!

Huo ndo ulikua mlipuko wa ndege wawili wapendanao kwa dhati; Bw Julianus Andrew Mambe na Bi Esther Brown Mwamafupa walipokua wakiingia kwa mbwembwe pale katika ukumbi maarufu jijini Dar es Salaam, Banora. Hapo wakiwa na uhakika wa kuishi pamoja mpaka kifo kitakapowatenganisha kama walivyoapa mbele ya waumini na mapadre wa Kanisa la Katoliki-Makuburi.

Huku wakisindikizwa kwa show ya hatari ya mabest friend; Emma, Eddy, Bruno, Lucas na mabinti kadhaa.na pembeni yao wapo wasimamizi wa ndoa na harusi hiyo; Bw Keneth Mvili na mkewe kipenzi, Praxeda.

Siku hiyo ambayo ilikua maalum pia kwa mdogo wake na Bwana harusi aitwaye Lilian John, aliyepata kipaimara na maharusi wakamlisha keki kama zawadi yao kwake.

DJ smol akiwapoteeza kabisa kwa uhondo wa wenyeji wote kutoka kule Ngoreme, serengeti na Kyela, Mbeya..za dini..kwaito....za zamaaaani na mijisebene na miduara...na weeeeee!! Bwana harusi akajikuta amenogewa na kuyarudi katikati ya wadau na huku akipigiwa makofi ya kutosha!! burudaani juu ya burudani ikiongozwa na sauti adimu ya dhahabu kutoka kwa mtanashati...Ze Blogger! YOUR SATISFACTION IS OUR PASSION

Songa nasi kwa picha

Colours: sivler na Navy Blue